airport jogging

mavazi

aus521

aus9

Tuesday, November 11, 2014

AFARIKI KWA KUGONGWA NA BAISIKELI

AFARIKI KWA KUGONGWA NA BAISIKELI

Ndugu  wa  kijana  Daniel aliyegongwa na Baiskeli na kufa  wakilia kwa  uchungu  eneo katika  barabara  kuu ya Iringa- Mbeya eneo la Kitwiru mjini Iringa ambako ajali  hii  imetokea kwa daladala  ya Iringa- Mafinga  kumgonga  kijana  huyo hadi kufa
Baiskeli  aliyokuwa akitumia marehemu  ikiwa  imeharibika  vibaya  baada ya kugongwa na daladala  eneo la Sapria Kitwiru mjini Iringa leo  mida ya saa 2 usiku
Mkuu  wa  Trafiki mkoa  wa Iringa  akiwa  eneo la  tukio  akiangalia  mwili  wa  kijana  Daniel aliyekufa kwa  kugongwa na daladala  leo
Askari  wa  usalama  barabarani  wakifika  eneo la tukio  kuchukua mwili  wa marehemu  Daniel mkazi  wa Njombe aliyegongwa na  gari  usiku  huu
Mwenyekiti  wa CCM  mkoa  wa Iringa  Bi.Jesca  Msambatavangu  mtu  wa  watu  wa pili  kulia akiwa katika  eneo la  tukio   kuomboleza  msiba huo  usiku  huu ni kiongozi pekee  aliyefika  kuungana na wananchi hao wa eneo la Kitwiru katika  shida  hiyo
hapa  mkuu waTrafiki mkoa  wa Iringa akiungana na wananchi kusaka  vioo  vilivyovunjika  ili kupata  ushahidi
Hii ni Baiskeli  aliyokuwa akitumia marehemu kabla ya  kifo  chake  ikipakiwa katika  gari ya  polisi
Mwili  wa  kijana  Danieli  ukiingizwa katika gari ya  polisi





 Kijana mfanyakazi  wa ndani katika  eneo la Kitwiru  mjini  Iringa  aliyefahamika kwa jina mmoja la Daniel mkazi  wa  mkoa wa Njombe amekufa  papo hapo  baada ya kugongwa na  daladala  lililokuwa  likitokea  mjini  Iringa  kwenda  Mafinga  wilaya ya  Mufindi.

Wakizunguza na mtandao  huu  wa www.francisgodwin.blogspot.com na www.matukiodaima.com  mashuhuda  wa  tukio  hilo  wamesema kuwa  kijana  huyo aligongwa  mida ya saa 2 usiku  wakati akitoka  kupeleka maziwa kwa mteja  eneo la Ruaha na  wakati akirejea  nyumbani ndipo  alipogongwa na daladala hilo  lililokuwa katika mwende kasi  likitoka  mjini Iringa kwenda  Mafinga .

Hata  hivyo  walisema  baada ya  daladala  hilo kumgonga halikuweza  kusimama zaidi ya  kuongeza mwendo na kuendelea na safari .

Pia  walisema  mwili  wa kijana  huyo ulikutwa na simu  huku  masikioni akionekana kuwa na vifaa maalum vya  kumwezesha  kusikiliza muziki kutoka katika  simu na kuwa yawezekana  ajali  yake  ilisababishwa na  muziki aliokuwa akisikiliza kijana  huyo na kushindwa kusikia honi ambavyo dereva  wa daladala  hilo alikuwa a

No comments:

Post a Comment