airport jogging

mavazi

aus521

aus9

Tuesday, November 18, 2014

AISHA BUI KUBURUZWA KORTINI

KESI ya msanii wa filamu Bongo, Aisha Bui ya kufanya fujo ofisini kwa msambazaji wa filamu akidai kutolipwa fedha zake za filamu bado ni ya moto ambapo msambazaji anazungumza na mwanasheria wake kisha kumburuza mwigizaji huyo mahakamani.
Msanii wa filamu Bongo, Aisha Bui wakati akiwa katika ofisi za kusambaza filamu za Yuneda zilizopo Mbagala.
 
Chanzo makini kimedai kuwa, baada ya Aisha kulala polisi na kutoka kwa dhamana msambazaji huyo, Ngeze Yuneda anatarajia kumburuza mahakamani akidai amembambikizia madai mengi ya uongo.
Alipoulizwa Aisha kuhusiana na habari hiyo, alisema:
“Hata sielewi kwa sababu walisema wanapeleka faili kwa mwanasheria ndipo tutakapoitwa ili ijulikane inakuwaje, nawasubiria.”
Aisha Bui akiwa mwenye gadhabu siku ya tukio.
Hivi karibuni Aisha alifanya fujo kwenye ofisi za Yuneda kutokana na kumuuzia muvi tangu Aprili, mwaka huu lakini hakumpa fedha yoyote na walikubaliana milioni tisa lakini alikuwa akimpiga kalenda ndipo akamwangushia timbwili ofisini kwake.

No comments:

Post a Comment