airport jogging

mavazi

aus521

aus9

Wednesday, November 12, 2014

Beyonce: Uzuri wa nje huwa unachuja


Marekani. Mwanamuziki Beyonce anafahamika kwa umahiri wake wa kuteka vyombo vya vya habari wakati mwingine bila hata kufungua kinywa chake. Ndoa yake, ujauzito wake na kuachia albamu kimyakimya ni mambo ambayo yamewahi kuvunja rekodi za kuandikwa mara nyingi huku mwenyewe akibaki kimya.
Katika mahojiano na Jarida la Bazaar, ‘supastaa’ huyo anafunguka kuhusu upande mwingine wa maisha yake katika muziki, fasheni na familia.
Bazaar: Kama ukipewa nafasi ya kurudi utoto ni kitu gani utafanya?
Beyoncé: Nitaiamuru nafsi yangu ijiamini. Sasa hivi nimefikia katika hatua ambayo sijali watu wengine wanasema nini juu yangu. Nilipokuwa mdogo kila nilichofanya kwanza nilitaka kujua, je, watu watanichukuliaje.
Bazaar: Mara nyingi umekuwa ukisema wewe ni mtu mwenye aibu, lakini katika kazi zako unaonekana unajiamini, hii ikoje?
Beyoncé: Sasa hivi sina aibu sana kama ilivyokuwa zamani. Mimi ni mtu ninayependa zaidi kusikiliza kuliko kuongea ndiyo maana naonekana kuwa na aibu. Ninajiamini, ninapenda ninachofanya na ninajituma haswa.
Bazaar: Unawataja Diana Ross na Tina Turner kama unafuata nyayo zao, kitu gani hasa unakipenda kutoka kwao?
Beyoncé: Walikuwa ni wanawake waliojituma bila waoga. Kumbuka
pia
wanawake hawa waliofanikiwa kuchomoza katika jamii ambayo ilikuwa ikimdharau mtu mweusi.
Bazaar: Uko karibu sana na mdogo wako Solange, lakini aina ya maisha yenu ni tofauti, ni kitu gani kinawaunganisha?
Beyoncé: Kwanza kama ulivyosema Solange ni mdogo wangu. Ninampenda sana na nafikiri tofauti zetu katika mambo tunayoyapenda na kuamini ndiyo inayotuunganisha.
Bazaar: Ushauri gani mzuri ambao mama yako amewahi kukupa?

No comments:

Post a Comment