airport jogging

mavazi

aus521

aus9

Wednesday, November 12, 2014

mwanzo Burudani Burudani ‘Niliigiza mcharuko kuwakata ngebe mtaa wa pili’


Mcheza filamu Shamsa Ford amesema kuwa alitunga filamu ya Chausiku kuonyesha uwezo walionao baada ya kunangwa kuwa ‘anauza sura’ katika tasnia hiyo.
Ford alisema mara nyingi kumekuwa na maneno kuwa waigizaji wasiopitia katika vikundi kama cha Kaole Sanaa Group, kazi yao ni kutafuta umaarufu, shutuma za karibuni zikiwa zimetolewa na Nuru Nasoro, maarufu kwa jina la Nora, ambaye aliwaelezea waigizaji wanaochipukia kuwa ni “wauza sura” na hawana jipya.
Lakini Ford alisema kauli hiyo na nyingine nyingi za kuwabeza, zilimuhamasisha kufanya kitu ili kuonyesha kuwa wanachotaka kufanya kazi ndiyo maana akaibuka na filamu hiyo.
Alisema kwa kawaida yeye ni mpole sana, lakini katika filamu hiyo ameigiza mcharuko na asiyekwenda na wakati.
“Nakumbuka nilikuwa nimepumzika ufukweni nikiawaza ni kwa jinsi gani nitaweza kuonyesha uwezo wangu binafsi. Kuigiza, naigiza sana tu, lakini bado kazi yangu haionekani, badala yake naonekana muuza sura,” alisema Ford.
Akizungumzia filamu hiyo ambayo ni gumzo hivi sasa, Ford alisema ametunga mwenyewe na inasimamiwa na kampuni ya Jerusalem Film.
“Hata sisi tunaweza na vipaji tulizaliwa navyo, lakini wakati haukuruhusu kujikita kwenye mambo hayo na tulipopata nafasi tumeweza kuonyesha jinsi gani tunaweza na bado wasubiri kutuona zaidi na zaidi; huu ni mwanzo, ”alisema Ford.
Ford alisema licha ya kuwa na tabia ya upole, hakupata shida kuigiza katika nafasi ya mcharuko kwa kuwa lilikuwa ni wazo lake na aliyelitekeleza ni yeye na kwamba kama isingekuwa hivyo, ingemchukua muda kidogo kuelewa mtunzi alikuwa anataka nini, kwa kuwa siyo kitu cha kufikiria harakaharaka.

No comments:

Post a Comment