IMEVUJA! Kumbe rapa mwenye jina
kubwa Afrika Mashariki, Jackson Makini ‘Prezzo’moja ya ishu zilizomleta
Bongo ni pamoja na kukutana na muuza nyago kwenye Video za Kibongo, Gift
Stanford ‘Gigy Money’.
Akichonga na mtandao huu, Prezzo
aliyewahi kubamba na Ngoma ya Nipe Nikupe akimshirikisha staa wa Bongo
Fleva, Ambwene Yessaya ‘AY’ alisema kuwa, Gigy ni msichana ambaye
amekuwa akimsikia siku za hivi karibuni Wakenya wakimzungumzia hasa juu
ya vituko vyake jambo lililomfanya kuvutiwa kuonana naye.
“Gigy yuko hot mazee, nimemsikia sana
Wakenya wakimzungumzia so nipo katika mpango wa kuonana naye, si unajua
mimi nina mambo mengi, reality show na vitu vingine private,” alisema
Prezzo. Gigy Money aliponyetishiwa ishu hiyo alifurahia jina lake kupaa
hadi Kenya.
No comments:
Post a Comment