airport jogging

mavazi

aus521

aus9

Tuesday, June 7, 2016

Tukio la Ajabu Kaburini

kaburi

DAR ES SALAAM! Wakazi wa Mbagala Chalambe jijini Dar es Salaam, waliamka asubuhi na kukutana na tukio lililojaa maswali mengi huku majibu yakiwa haba kufuatia kukuta kitu kaburini kikiwa kimeviringishiwa sanda.
ILIVYOKUWA
Kwa mujibu wa shuhuda wetu, tukio hilo lilijiri hivi karibuni kwenye Makaburi ya Chalambe ambapo wakazi hao walilizunguka kaburi hilo huku wakidai kuwa, ndani ya sanda hiyo kulikuwa na mtoto aliyeuawa na kuwekwa hapo.
SHUHUDA ATOA
MAWAZO YAKE
“Jamani humu kwenye sanda kuna maiti ya mtoto mdogo. Lazima kuna mahali ameuawa, wakamviringishia sanda maskini wa Mungu, wakaja kumuweka hapa,” alisema mkazi mmoja akiwa amejikunyata baada ya kutoka kulala.
IMG-20160522-WA0001MTAZAMO WA WENGINE
Wengine walisikika wakisema kuwa, kwa vyovyote mtu au watu waliotupa kitu hicho walikuwa katika harakati za ushirikina kutokana na maelekezo ya mganga.
“Huu ni ushirikina mkubwa, lazima watu wamefanya hivi kwa maelekezo ya mganga. Huwezi kuja kutupa vitu vya uchawi kwenye kaburi la mtu, watu hawana hata woga wala hawamuogopi Mungu,” alisema mama mmoja.

POLISI WAITWA
Ili kutatua kitendawili hicho cha nini kilikuwa ndani ya sanda, baadhi ya wananchi walikwenda Kituo cha Polisi Mbagala Chalambe na kuripoti tukio hilo ambapo baadhi ya askari waliongozana na watoa taarifa hao mpaka eneo la tukio.
Baada ya polisi kufika, macho ya kila mtu yalikuwa na shauku ya kutaka kuona ndani ya sanda ile mlifungwa nini ili waanze kutoa mitazamo yao.
KILICHOKUTWA
Hata hivyo, katika hali isiyokuwa ya kawaida, baada ya polisi kuifungua sanda hiyo, kilichokutwa ndani ni jogoo wawili ambao walikuwa hawana vichwa!
Watu walitawanyika, wengine wakisikitika, wengine wakicheka lakini wapo pia waliokuwa wakilaani tendo lile hasa kwa kuzingatia kuwa, lilifanywa juu ya kaburi la marehemu ambaye ana ndugu zake walio hai hivyo kuzidisha majonzi kwao.
MZEE ALAANI
Mzee mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Ally Mwanaisi akizungumzia tukio hilo, alisema dunia ndiyo imefikia hapo, kwamba watu hawaogopi kufanya lolote.
“Hii ni dunia ya mwisho. Mtu anakuja kufanya ushirikina wake kwenye kaburi la mwenzake bila woga. Hivi hao waganga ndiyo wanawaambia kwa kufanya hivi mambo yao yatakuwa mazuri siyo?” alihoji mzee huyo.

No comments:

Post a Comment