aus9
Wengi wanamjua kwa jina la Nikita kutoka kwenye kiwanda cha filamu
Bongo lakini jina lake halisi ni Elizabeth Chijumba, mwanamke
aliyefanikiwa kufanya vizuri kwenye filamu mbalimbali zikiwemo za
mapigano kama vile CID, We Are Four, Stolen Will, Well Done My Son na
Adela.
Nikita ambaye ni mke wa msanii Khalfan Ahmad ‘Kelvin’ (mume wa zamani
wa Yobnesh Yusuf ‘Batuli’) ni mwanamke pekee Bongo anayefanya vizuri
kwenye filamu za mapigano.
Historia yake kwa kifupi
Alizaliwa mwaka 1982, elimu ya msingi
akasoma Oysterbay Primary School ya jijini Dar kabla ya kuhamia Mzumbe
Shule ya msingi iliyopo Morogoro.Baadaye alirudi tena jijini Dar katika
shule ya msingi Kizuiani iliyopo Mbagala kufuatia baba yake kuhamishiwa
kikazi. Hapo akahitimu darasa la saba mwaka 1995.
1996 alianza Shule ya Sekondari Vosa Kongowe, akamaliza mwaka 1999 na safari yake kielimu ikaishia hapo.
Anusa umiss
Kwenye mambo ya urembo, Nikita anasema; “Mwaka 2000
nilijitosa kwenye Miss Kinondoni lakini kutokana na ufupi wangu
niliambulia taji la Miss Kimara kisha safari ikaishia hapo.”
Ndoto za uigizaji zaanza
“Nilikuwa na ndoto za kuwa muigizaji
hivyo niliamua kuwatafuta baadhi ya mastaa enzi hizo kama vile JB lakini
sikufanikiwa kushaini.”
Ajiunga na chuo cha DSJ
“Mwaka 2003 nilijiunga chuo cha
uandishi wa habari cha DSJ ambapo nilikutana na msanii wa Kundi la Sanaa
Group aitwaye Dina ambaye siku moja aliniomba nimsindikize mazoezini,
huko nikakutana na JB, akanipenda na kunipa kazi ya kwanza, nakumbuka
ilikuwa ikiitwa Kanisa la Leo, hapo ukawa mwanzo wa mimi kuigiza.”
Magumu anayokutana nayo
“Kwa sasa nacheza sana filamu za action
hivyo changamoto ni nyingi kwani nafanya na wanaume, natumia nguvu sana,
kuna wakati naumia kweli lakini kwa sababu ni kazi ninayoipenda,
naendelea kupambana.”
Mume anamchukuliaje
“Tukiwa kazini ni kazi, nikiumia ananihudumia
kama wasanii wengine kwa sababu yeye ni dairekta, ila tukifika nyumbani
anakuwa mume na mambo mengine yanaendelea kama kawaida.”
Mafunzo ya judo
“Sijawahi kupitia chuo cha judo ila mume wangu
ambaye ndiye kiongozi wangu amekuwa akinifundisha sana staili hizo na
sasa nimewiva kwa kiasi flani.”
Ashawishiwa na Cynthia Rothrock
“Msanii wa nje Cynthia Rothrock
ndiye aliyenishawishi mpaka nikaamua kucheza filamu hizi kwani
nilijiuliza kwamba, kama yeye ameweza na mimi nitashindwaje?”
Amzungumzia Batuli
Alipoulizwa kuhusiana na uhusiano wake na
Batuli ambaye aliachwa na Kelvin kisha akaolewa yeye, Nikita alisema
kuwa anamheshimu, kwanza kama msanii mwenzake na pia mzazi mwenzake na
mumewe.
“Tukikutana tunaongea vizuri tu na mwanaye namlea kama wangu, namheshimu ananiheshimu,” alisema Nikita.
Atoa la moyoni
“Nawasihi mashabiki waangalie kazi za msanii siyo
kuangalia kashfa. Mimi ninao uwezo wa kucheza filamu nyingi lakini
waongoza filamu ‘madairekta’ ndiyo huwa wananipangia filamu za action na
nazipenda kwa sababu nimezizoea
No comments:
Post a Comment